Mgombea ubunge katika jimbo la Kawe, kwa tiketi ya chama cha upinzani CHADEMA Halima Mdee, amelalamikia udanganyifu katika kupiga kura ambapo anasema alishuhudia mwenyewe udanganyifu huo. Hata hivyo mwenyekiti wa tume ya uchaguzi nchini Tanzania Jaji Semistocles Kaijage amesema mbele ya waandishi wa habari kuwa taarifa za kukamatwa kwa kura feki ni uzushi na siyo za kweli. Kurunzi 28.10.2020